Ndege ya Kenya yaanguka Somalia na kusababisha vifo vya watu 6

plane 1
plane 1
Watu sita wameaga dunia baada ya ndege moja iliyosajiliwa Kenya kuanguka nchini Somalia.

Wizara ya mashauri ya kigeni nchini imeitaka Somalia na  mashirika ya kimataifa kuchunguza kikamilifu kuanguka kwa ndege moja ya  kampuni ya kibinafsi iliyokuwa ikisafirisha misaada ya kupambana na virusi vya corona.

Ndege hiyo ilianguka katika hali ya kutatanisha  katika eneo la Bardale, Baidoa nchini Somalia siku ya Jumatatu tarehe 4. Kenya imeyataka mashirika mengine ya ndege yanayohudumu katika eneo hilo kuchukua tahadhari  kwani hali  iliyosababisha ajali ya ndege hiyo bado haijaeleweka .

Wizara ya mashauri ya kigeni ya Kenya imesema itashirikiana na mashirika mengine kufuatilia kwa karibu uchunguzi  kuhusiana na  tukio hilo na kutafuta suluhisho. Ndege hiyo yenye nambari ya usajili 5Y-AXO ilikuwa ya kampuni ya  African Express na ilisababisha vifo vya watu wote sita waliokuwemo .