Hazina ya kitaifa ya matibabu NHIF itagharamia huduma za matibabu ya wagonjwa wa virusi vya coona katika hospitali za umma .
Kupitia taarifa kutoka kwa afisa mkuu mtendaji Peter Kamunyo ,NHIF imesema itawasaidia wote waliopatikana na virusi hivyo na waliolipiwa ada za kila mwezi ambao watalazwa katika hospitali zilizoidhinishwa na wizara ya afya .
Hospitali hizo ni ; Kenyatta National Teaching and Referral Hospital, Kenyatta University Teaching Referral ,Research Hospital na Mbagathi County Hospital.
Nyingine ni hospitali za kaunti na taasisi nyingine za matibabu zenye idhini ya kuwahudumia wagonjwa wa Covid 19
"NHIF haitagharamia bili zitokanazo na kulazwa katika hopitali ambazo hazijaidhinishwa na wizara ya Afya’ amesema Kamunyo .
,wezi machi kampuni za kutoa huduma za bima zilikubali kugharamia matibabu ya coronavirus baada ya mashauriano .