Masaibu yake yalianza wakati alipoanza kuugua na kisha kupimwa na kupatikana na saratani ya sehemu yake ya uume. Iligunduliwa kwamba kansa ilikuwa imeathiri sehemu kubwa ya uume wake na chaguo lilikuwa kuikata kabisa kupitia upasuaji kwa jina la kiingereza Penectomy. Hakuamini alipoarifiwa habari hizo na alipewa muda wa kuamua endapo angeidhinisha oparesheni hiyo au la kwa sababu endapo uume wake haungekatwa basi ingekuwa mwisho wa maisha yake. Baada ya majadiliano na familia yake na kubainika kwamba hapakauwa na njia nyingine iliamua kwamba oparesheni hiyo ingefanyika na akahamishwa kwenda katika hospitali moja India ambako upasuaji wa kuukata uume wake ulifanyika. Upasuaji wenyewe ulihusisha kuonodoa uvimbe uliokuwa ndani ya misuli ya sehemu hiyo na hata mizizi inayoshikilia uume wake kwa mwili iling’olewa.
Bila kujua kitakachofuatia, mkewe Victor hakuwa amejitayarsha kuishi na mume asiyeweza kumpa tendo la ndoa na kwa bahati nzuri, Victor alikuwa na watoto wawili aliopata kabla ya kupata kansa. Miezi miwili tangu aliporejea nchini na kuanza kupata nafuu, wengi walishangaa jinsi Victor na mkewe wangeendelea kuishi pamoja kama mke na mume hasa baada ya upasuaji huo.‘ Kilichofanya mke wangu kuniacha ni maswali ya mara kwa mara kutoka kwa watu wakiwemo majirani waliotaka kujua iwapo kuna njia ya mimi naye kuendelea kushiriki tendo la ndoa,’ anasema Victor.
Anasema alifikiri baada ya miaka 10 ya ndoa walikuwa wamejenga uhusiano thabiti ambao haungetikiswa na oparesheni aliofanyiwa kumbe hakujua umuhimu wa tendo la ndoa kwa mkewe. Kuondoka kwa mkewe ghafla kumemuacha Victor katika hali ya kutojifahamu kwani haamini kwamba licha ya kutatizika kiakili kwa ajili ya kukatwa uume wake, sasa pia atasalia bila mke na katika hali yake itakuwa vigumu kumpata mwanamke atakayeishi naye kutokana na hali yake. Je, ungejipata katika hali ya Victor ungefanya nini?