Omar Lali, mpenzi wake marehemu Tecra Muigai ashtakiwa kwa mauaji

Omar Lali,  mpenzi wa  mwanawe mmiliki wa Kampuni ya Keroche  Tabitha Karanja, Tecra Muigai ameshtakiwa leo  huko Lamu kwa mauaji yake.

Tecra aliaga dunia mei tarehe 2  katika nyumba moja ya kibinafsi huko Shella, kaunti ya Lamu alikokuwa akiishi na Lali.

Baada ya kuanguka inaarifiwa kwamba alipelekwa katika hospitali moja ya eneo hilo kabla ya kusafirishwa kwa ndege hadi Nairobi kwa matibabu lakini akaaga dunia  kutokana na majeraha aliyopata.

Lali alikamatwa baadaye kutokana na kifo cha Tecra  kwa kushukiwa kwamba ndiye aliyemsukuma.

Kulikuwa na ripoti kwamba palikuwa na ugomvi kati yao  kabla ya kifo chake, madai ambayo wakili wa bwana Lali anayakana vikali.

Mwezi mei, mahakama ilikataa  ombi la kutaka kundelea kumzuilia Lali seli   kabla ya kushtakiwa kwake.