PATANISHO: Mke Wangu Aliondoka Alipogundua Nina Mpango Wa Kando

Felix alituma ujumbe akiomba apatanishwe huku akidai mkewe aliondoka baada ya kugundua kuwa ana mpango wa kando.
'Bibi yangu Cate nilimuoa akiwa na watoto na tumevumiliana na sasa watoto wamekuwa wakubwa. Mimi ni mpishi na siku moja katika hali ya kuchokora simu yangu aligundua kuwa kuna wanadada nimekuwa nikizungumza nao.

Sasa akapata msichana fulani ambaye tulijuliana Facebook na ilifika wakati nikama tulikuwa tunatongozana. Sasa mke wangu akakasirika na akaondoka na hadi wa leo hajawahi rudi na hajibu simu zangu." Alieleza Felix.

Alipopigiwa simu bi Cate, alidai mumewe alimtishia akidai kuwa ataharibu watoto wake.

&feature=youtu.be