PATANISHO: Mwanadada Huyo Asipomuacha Bwanangu Nitahakikisha Nimemueka Kaburini

Betty alituma ujumbe akidai kuwa kuna msichana anataka kuharibu ndoa yake huku akitaka awachane na mume wake.

"Nataka tu kumkanya awachane na mume wangu kwani alipiga simu usiku nikachukua na nikamwambia kuwa mimi ndiye mke wa mzee na awachane naye. Lakini siku iliyofuata bado nikampigia na nikamkanya.

Shida ni eti bado aliendelea na ile tabia licha ya mume wangu kukiri na kuomba msichana. Uhusiano wao umekuwa ukiendelea kwa miezi minane." Alijieleza Betty.

Alipopigiwa simu bi Claire alidai kuwa ameolewa na hana mwanaume mwingine nje ya ndoa yake wala hamjui mama Betty.

Baada ya kusema yale bi Claire alikata simu aliposkia sauti ya Mama Betty.

"Nitamtembelea azikwe na wazazi wake walie akiwa kaburini, nitahakikisha yale kwani haskii. Nitamweka kwa mchanga ndio roho yangu itulie." Alisema mama Betty akiwa na wingi wa hasira.

Pata uhondo kamili.

&feature=youtu.be