PATANISHO: Nashuku mume wangu ataniua kwani ashawahi nidunga na kisu

Bwana Koech ndiye aliyeomba kupatanishwa hii leo na mkewe bi Carol ambaye walikosana mwezi wa Disemba.

Nilikuwa nimesafiri siku moja na tulipowasiliana naye kwa simu hatukuelewana na nilimskia akiamsha watoto usiku ili waondoke. " Alisimulia Koech.

Aliongeza,

Niliporudi nyumbani nilipata mbwa amefungia kwa nyumba, paka analia, picha zimetapakaa kwa nyumba na nguo zangu Imeraruliwa.

Wawili hao wamekuwa kwa ndoa ya miaka 11 na wamejaliwa watoto wawili ambao aliondoka nao.

Anasema sasa hivi, Carol anaishi dadake Kabarnet na mara ya mwisho kuzungumza alikuwa anaomba nauli ya gari lakini anashuku kuwa anahitaji fedha za kuhama kwa dadake.

"Mimi najua alikuwa ananidanganya kwani alisema yuko kakamega lakini kwa damu yangu nilihisi alikuwa karibu. " Alisema Carol.

Aliongeza,

Alinidunga na kisu kichwani na mkono na sasa hata nikimsamehe nitaogopa kuwa ataniua tukirudiana. "

Hata hivyo Carol anasema kuwa mumewe hafai kuogopa kuwa mkewe hatorudi akitumiwa fare, akiongeza yeye amelelewa ki ukristo.