PATANISHO: Nilimuuma mke wangu kifuani kwa hasira

Bwana Musa alituma ujumbe akiomba apatanishwe na mkewe, bi Barbra, akidai kuwa walikosana na kwa hasira akaamua kumuuma na kupelekea mkewe kupotea.

"Tulikosana nikapandwa na hasira nikamuuma na akatoroka. Nilimuuma upande wa chini karibu na matiti, lakini namuomba msamaha." Alieleza Musa.

Tulikosa trust kati yetu kwani nilikuwa namshuku kuwa ana mpango wa kando kwani alikuwa na madharau kwa nyumba na hatukuwa tunaelewana. " Alieleza Musa ambaye wamekuwa kwa ndoa ya miaka minane.

Tangia aondoke, wawili hao wamekuwa kwa mazungumzo lakini hadi wa leo bado hawajaweza kusuluhisha malumbano yao.

Wawili hao walijaliwa wana watatu lakini mmoja aliaga dunia.

"Mimi sahii nimeshapata kazi, nimepeleka watoto shuleni. Sahii unadhani mimi ndio nitakuwa mzuri au wewe?" Alisema Barbra akimkumbusha kuwa amekuwa akimsamehe mara kwa mara.
Pata uhondo kamili.

&feature=youtu.be