PATANISHO: Nina tabia ya kupiga mke wangu Manchester United ikipigwa

Samuel alituma ujumbe akiomba apatanishwe na mkewe Wambo akidai kuwa pombe ndio iliwakosanisha kwani alikuwa anakunywa vibaya sana. Isitoshe, yeye ni shabiki sugu wa Manchester United na kila wakati wanapofungwa yeye huleta vita.

"Unajua mtu hupewa mawaidha, niliambiwa nikifika kwa nyumba nikipata ana kelele naondoka naenda kutuliza mawazo na hapo nikaanzisha moto mwingine." Alieleza Sammy.

Nililala nje na nikawa nimemwachia fedha alipe nyumba na hakulipa, kumoigia simu kumuuliza mbona ma ajenti wako area alisema kuwa alikuwa barabarani akielekea Naivasha. Nilijaribu kumbembeleza ingawa anirudishie fedha kadhaa akasema kuwa ana watoto wangu na hawezi nirudishie." Aliongeza Sammy mwenye umri wa miaka 44.

Wawili hao wamekuwa kwa ndoa ya miaka sita na wamejaliwa watoto watatu.

Wambui alipopigiwa simu alidai kuwa bwanake ana tabia ya kunywa sana na kuwafukuza pamoja na watoto nje usiku wa manane.

"Nilitoka kwake kwani alisema kuwa akipata siko kwa nyumba yake ndio atafurahi sana na nikaondoka. Kila wakati akiingia kwa nyumba huingia na vita na husema atabadilika na hajawahi badilika." Aliongeza Wambo.

Pata uhondo kamili.

&feature=youtu.be