PESA ‘OTAS’! Mfahamu Bilionea wa Zimbabwe atakayewalipa madaktari nchini humo kwa miezi 6

Strive
Strive
  Bilionea Strive Masiyiwa  raia wa Zimbabwe anayeishi  Uingereza amesema atawalipa madaktari nchini Zimbabwe kurejea kazini baada ya mgomo ambao umedumu zaidi ya miezi minne. Lakini wengi  wana maswali mengi kumhusu Masiyiwa ambaye ameahidi  kumlipa kila daktari  marupurupu ya  dola 230 na kuwapa nauli ya kwenda kazini kupitia hazina aliyoanzisha .

Mgomo huo wa madaktari nchini Zimbwabwe umesababisha vifo vya watu kadhaa  na umekuwa mojawapo ya migomo iliyodumu muda mrefu sana nchini humo. Bwenyenye huyo  amewapa madaktari ofa hiyo nzuri na wemekubali kurejea kazini. Madaktari wengi  wanaoshiriki mgomo huo hulipwa chini ya dola 100 kwa mwezi . Ufadhili wa bilionea huyo utadumu kwa miezi sita lakini haijafahamika kitafuata kipi baada ya  muda huo.

Madaktari wanaogoma wamekuwa wakitaka kuongezwa mishahara ili kuweza kukimu gharama iliyopanda ya maisha nchini humo kwa ajili ya hali mbaya ya uchumi wa Zimbabwe .

 Strive Masiyiwa ni nani?

Mzaliwa huyu wa Zimbabwe alizaliwa mwaka wa 1961  na kwa sasa anaishi  mjini London. Ni mmiliki wa kampuni ya mawasiliano ya Econet Wireless. Mali yake inakadiriwa kuwa na thamani ya  Dola za kimarekani  bilioni 1.1(mwaka wa 2020).