Mnamo mwaka wa 1955 Moi alijitosa katika siasa alipochagliwa katika bunge ili kuliwakilisha eneoe la Rift valley katika LEGCO.Aliteuliwa kuichukua nafasi ya Dr.John Ole Tameno mwakilishi wa zamani aliyeng’atuka maamlakani kwa sababu ya unywaji pombe kupindukia na kushukiwa kuhusika na vugu vugu la kupigania uhuru . Mwaka wa 1957 Moi alichaguliwa tena kujiunga na legco na akawa waziri wa elimu katika serikali ya kabla ya Kenya kupata uhuru kati ya mwaka wa 1960–1961. Mwaka wa 1960 alikuwa miongoni kwa walionzisha chama cha KADU pamoja na Ronald Ngala ili kupigania uongozi dhidi ya chama cha KANU kikiongozwa na Mzee Jomo Kenyatta .KADU ilipigania kuwepo kwa utawala wa majimbo ilhali Kanu Ilitaka pawepo serikali ya muungano na utawala wa kikapitolisti . Kanu hata hivyo ilikuwa na uthabiti wa idadi ya waakilishi pamoja na kuungwa mkono na Uingereza amayo ilichukua hatua za kuondoa vipendee vyote vya majimbo katika katiba
Mnamo mwaka wa 1978 Moi alichukua usukani wa kuiongoza nchi wakati mzee Jomo Kenyatta alipoaga dunia .Aliongoza hadi mwaka wa 2002 alipostaafu . Kupitia shinikizo la mageuzi ,Moi aliruhusu kuwepo mfumo wa siasa za vyama vingi mwaka wa 1991 na kukiongoza chama cha KANU kupata ushindi katika chaguzi za 1992 na 1997 . kabla ya kuwa rais Moi alihudumu kama makamu wa rais kutoka mwaka wa 1967 hadi 1978 .Moi alimua kuendeleza mfumo wa ‘nyayo’ ili kudumisha sera na mtindo wa utawala wa mtangulizi wake Mzee Jomo Kenyatta . Pia alipata jina la sifa kama ‘profesa wa siasa ‘ kwa sababu ya uongozi wake uliodumu miaka 24 na jinsi alivyokabiliana na wapinzani wake .Akiwa na umri wa miaka 95 Moi alikuwa rais mstaafu mwenye umri wa juu zaidi aliyekuwa hai. Februari tarehe 4 2020 ,Daniel Arapa Moi aliaga dunia katika hospitali ya Nairobi . Mwezi uliopita madaktari katika hospitali ya Nairobi walilazimika kumrejesha Moi katika mashine za kumpa usaidizi wa kupumua .Hali yake ya afya imekuwa maaya tangu oktoba mwaka jana alipolazwa hospitalini .
Wakati huo alipolazwa hospitalini ,msemaji wake Lee Njiru alisema Moi alikuwa amekwenda hospitali kwa ukaguzi wa kawaida lakini tangia hapo alilazwa hospitalini mara nne. Kundi lake la madaktari likiongozwa na Daktari David Silverstein limekuwa likimpa mkatibabu kwa matatizo yanayojirejeeza na kumfanya kusalia kitandani kwa miezi mitatu . Hali ya afya ya Mzee Moi ilizidishwa kuwa mbaya na jeraha la goti alilopata wakati wa ajali iliyohusisha gari lake mwaka wa 2006 huko Limuru . Mzee Moi angetimu umri wa miaka 96 Septemba mwaka huu