Wafanyikazi wanne raia wa Uchina wa kampuni moja ya ujenzi wamekamatwa huko Lodwar kwa kumshambulia mhandisi mmoja wa Kenya aliyekosoa kazi yao . Rodgers Imasia ambaye ni mkaguzi wa barabara kutoka KENHA Alivamiwa na wachina hao kwa kutilia doa kazi yao ya ujenzi wa sehemu ya barabara ya Loichangamatak – Lodwar.