Marehemu Zindziswa alikuwa bintiye rais wa zamani wa Afrika kusini Nelson Mandela na mkewe wa zamani Winnie Madikizela.
Kulingana na shirika la habari nchini humo la SABC Zindisziswa mwenye umri wa miaka 59 anayefahamika pia kwa jina Zindzi, aliaga dunia siku ya Jumatatu na kifo chake kutangazwa na wakfu wa baba yake, Nelson Mandela Foundation.
Zindzi aliaga dunia katika hospitali moja ya Johannesburg na sababu ya kifo chake haijatolewa.
Katika taarifa yake siku ya Jumatatu, rais Uhuru aliitikia familia hiyo ustahimilivu na faraja kutoka kwa Mola wanapoomboleza kifo cha mpendwa wao.
Mandela kabla ya kifo chake alikuwa balozi wa taifa lake nchini Denmark.
Gavana wa Nairobi Mike Sonko katika risala zake alimtaja Zindzi kama mwanasiasa aliyekuwa mpole na mcha mungu
Zindzi, alikuwa dadake mdogo Zenani Mandela na alizaliwa Desemba tarehe 23 mwaka wa 1960 katika eneo la Soweto. Amewaacha watoto wanne, Zoleka, Zondwa, Bambatha na Zwelabo.