Ruto: Nitaendelea kuwapigania mahustler,DP asema akiwa Kisii

Ruto kisii
Ruto kisii
Naibu wa rais  William Ruto amesema ataendelea kupigania haki za watu wa kawaida  huku akisema kila mkenya ana haki ya kupata huduma kutoka kwa serikali .

Ruto ambaye amewahutubia  wananchi katika mji wa Kisii amewarai  watu wa eneo hilo kumuunga mkono huku akiwakumbusha kuhusu kampeini za Jubilee alizofanya wakati wa uchaguzi

Ruto amesema  hatotikiswa na watu wanaomkosoa  na kulemaza jitiahada zake za kufanya mikutano yake  kwani kuna kazi nyingi ya kuwapa Zaidi ya vijana  milioni sita kazi na kuwaondoa katika umaskini wakenya milioni 17 . Ruto amekashfu tabsha zilizotokea mjini Kisii kabla ya kuwasili kwake ambapo makundi ya vijana wanaopinga mkutano wake walipambana na polisi .

‘Kuna watu wanasumbua askari kuwaambia wasimamishe mkutano hii na ile  ..hiyo ni ukumbafu’ amesema Ruto

Ameongeza kusema;

‘Wale wanasiasa wanataka kushindana na mimi Waachane  na polisi wakuje kiwanja wakutanane na mimi’

Mji wa Kisii mapema alhamsi ulikuwa kitovu cha makabiliano kati ya makundi ya vijana waliokuwa wakiandamana dhidi ya Ruto na kundi jingine la kumuunga mkono .  Ruto amedai kwamba vijana hao walikuwa wamelipwa kusababisha vurugu .

‘ Tumewaonyesha wale wanaotumia watu vibaya  na kuwanunua vijana tunawaambia shame on you’  Ruto amesema

Ruto ameandamana na  na viongozi mbali mbali akiwemo mbunge Sylvanus Osoro ,John Kiarie ,naibu gavana wa Kisii Joash Maangi, waakilishi kadhaa wa kaunti na viongozi mbali mbali wanaomuunga mkono .