Muigizaji na mwanahabari Makena Njeri amejipata akiteka nyara mitandao ya kijamii baada ya gari lake zito aina ya Mercedes Benz kupigwa picha zenye maandishi ya kusema kwamba ni ‘cheater’.
Maandishi hayo kwenye gari jeupe yanaonekana katika umbali wa mita 100 na huenda yaliandikwa na mtu ambaye awali Makena amehusiana naye katika uhusiano wa kindani sana .
Picha za gari hilo likiwa na maandishi hayo ‘Makena Cheater’ zimekuwa zikisambaa mitandaoni huku watu wakizungumza kuhusu aliyeandika .Makena ambaye alifurahi sana alipopata gari hilo lake aliandka katika kundi moja la WhatsApp la wamiliki wa magari Mercedes Benz kueleza faharai yake kuwa mmoja wa wamiliki wa gari kama hilo . Muigizaji huyo hajatoa tamko lolote kuhusu kuwekwa maandishi hayo kwa gari lake .