'Makena Cheater':  Gari La Makena lachafuliwa kwa maandishi kwa  madai ya penzi la pembeni .

Muigizaji na mwanahabari Makena Njeri  amejipata  akiteka nyara mitandao ya kijamii baada ya gari lake zito aina ya Mercedes Benz  kupigwa picha zenye maandishi ya  kusema kwamba ni ‘cheater’.

Maandishi  hayo kwenye gari jeupe yanaonekana katika umbali wa mita 100 na huenda yaliandikwa na mtu ambaye awali Makena amehusiana naye katika uhusiano wa kindani sana .

Picha za gari hilo likiwa na maandishi hayo ‘Makena Cheater’ zimekuwa zikisambaa mitandaoni huku  watu wakizungumza kuhusu aliyeandika .Makena ambaye alifurahi sana alipopata gari hilo lake aliandka katika kundi moja la    WhatsApp  la wamiliki wa  magari  Mercedes Benz  kueleza faharai yake kuwa mmoja wa wamiliki wa gari kama hilo . Muigizaji huyo hajatoa tamko lolote  kuhusu kuwekwa maandishi hayo kwa gari lake .