Serikali yatenga shilingi millioni 650 kukabili changamoto ya maji katika kaunti 23

chelugi
chelugi
Serikali imetenga shilingi milioni mia sita hamsini kukabili changamoto ya maji katika kaunti ishirini na tatu ambazo zimeathirika pakubwa

Waziri wa maji, Simon Chelugui amesema fedha hizo zinatumika kuhakikisha maji yanafikia mashinani kwenye kaunti zilizoathirika

Waziri huyo alitaka baraza la magavana kuona kwamba magavana wanakomesha uhasama wa umiliki wa vyanzo vya maji akisema ni raslimali ambayo haina mipaka

Chelgui amesema uwepo wa raslimali ya maji hauzingatii mipaka ya ki maeneo

Gavana wa Kakamega Wycliffe Oparanya ametaja uwepo wa idara nyingi zinazohusika na usimamizi wa maji kuwa sababu ya gharama ghali ya maji.

Oparanya anaitaka serikali ya kitaifa kuona kwamba inaondoa mzigo kwa mwananchi aweze kupata maji kwa bei nafuu.

Kwingineko

Imebainika kuwa idadi ya vijana wanaochukua mikopo kutoka kwa hazina ya vijana nchini ni ya chini mno ikilinganishwa na kaunti zingine.

Afisa mkuu mtendaji wa hazina hiyo Josiah Moriasi anasema vijana pia hukuosa kulipa mikopo yao huku akisisitiza haja ya serikali za kaunti kuwapa zabuni makundi ya vijana ili kujiendeleza.
Hazina hiyo imetoa takribani milioni 35 pekee za mkopo kwa vijana kaunti hiyo kwa kipindi Cha miaka 12.