Waziri wa maji, Simon Chelugui amesema fedha hizo zinatumika kuhakikisha maji yanafikia mashinani kwenye kaunti zilizoathirika
Waziri huyo alitaka baraza la magavana kuona kwamba magavana wanakomesha uhasama wa umiliki wa vyanzo vya maji akisema ni raslimali ambayo haina mipaka
Chelgui amesema uwepo wa raslimali ya maji hauzingatii mipaka ya ki maeneo
Gavana wa Kakamega Wycliffe Oparanya ametaja uwepo wa idara nyingi zinazohusika na usimamizi wa maji kuwa sababu ya gharama ghali ya maji.
Oparanya anaitaka serikali ya kitaifa kuona kwamba inaondoa mzigo kwa mwananchi aweze kupata maji kwa bei nafuu.
Kwingineko
Imebainika kuwa idadi ya vijana wanaochukua mikopo kutoka kwa hazina ya vijana nchini ni ya chini mno ikilinganishwa na kaunti zingine.