Kampuni hiyo inayaleta pamoja mashirika mbali mbali ya kifedha ambayo yameweka raslimali pamoja ili kuweza kutoa mikopo kwa wakenya .Mikopo ya ujenzi wa nyumba imekuwa ya gharama ya juu sana kwa wakenya wengi na serikali inatumai kwamba kampuni hiyo mpya itaweza kuziba pengo hilo na kumaliza uhaba wa nyumba unaoshudia kwa sasa nchini .
KMRC, itaanza oparesheni zake ikiwa na mtaji wa mwanzo wa shilingi bilioni 35 na ilianzishwa kama taasisi ya kifedha isiochukua akiba chini ya uangalizi wa benki kuu ya Kenya .
Mkopo wa kwanza kuipiga jeki kampuni hiyo ulitoka kwa benki ya Dunia iliyotoa shilingi bilioni 25 na Benki ya Maendeleo barani afrika iliyotoa shilingi Bilioni 10. Rais Kenyatta amesema mpango huo wa KMRC ni ushirikiano kati ya serikali na Sekta ya kibinafsi .