Akizungumza katika kikao na wanahabari huko Kisumu siku ya jumapili amesema kwamba ni ndoto kwa baadhi ya watu kumtaka ajiuzulu.
" Suala ambalo watu wanalitumia kunitaka nijiuzulu ni ndoto . wanaweza kuendelea kuota’ amesema
Aliendelea kusema kwamba hana mtoto aliye chini ya umri wa miaka 18 katika nyumba yake .hii ni baada ya video kusambazwa mtandaoni inayodaiwa kuwa ya mwanawe wa kiume akiwa katika karamu licha ya agizo la serikali kuzuia watu kungomana kwa hafla kama hizo.
" Kuhusu suala la video ya mwanangu akiwa katika karamu ..sina mtoto wa kiume aliye chini ya umri wa miaka 18 katika nyumba yangu hatua inayomaanisha kwamba wote ni watu wazima .mnaweza kuwafuata na kuwauliza’ Kagwe alisema
Kuhusu suala la covid 19 nchini Kagwe alisema vis avipya 599 vya ugonjwa huo viliripotiwa na kufikisha jumla ya visa hivyo kuwa 6,436.
Watu 1,062 pia amepona virusi hivyo na kufikisha idadi ya waliopona 12,961.
Hata hivyo watu 2 waliaga dunia na kufikisha jumla ya walioaga dunia kwa ajili ya virusi hivyo kuwa 420