Ufichuzi umetolewa kuhusu ajali mbaya ya barabarani iliyotokea mwishoni mwa wiki katika barabara ya Lang’ata iliysababisha kifo cha mwanamme mmoja . Mashahidi wanasema walimshauri asiondoke kutoka hoteli ya Weston akiwa mlevi na atulie kidogo au atafute mtu wa kumpeleka nyumbani lakini juhudi zao ziliambulia patupu .
https://twitter.com/YusufJumaKenya/status/1229349238301233152
Alifahamu kwamba alikuwa mlevi chakari lakini hakutaka usaidizi wa yeyote na akaliendesha gari la Mercedes-Benz kwa kasi. Hatima yake baadaye ilifahamika baada ya gari hilo kushika moto baada ya kugonga ua la uwanja mdogo wa ndege wa Wilson . Naibu OCPD wa Lang’ata John Samburumo amesema dereva huyo alikuwa akiliendesha gari hilo kwa kasi sana .
Amesema alikuwa akitoka hoteli ya Weston mwendo wa saa moja na dakika 20 asubuhi na alionekana kuwa mlevi. Gari jingine lililokuwa limeegeshwa ndani ya uwanja wa ndege wa Wilson pia liligongwa . Gari hilo baadaye lilishika kasi upande wa mbele .Mwili wake ulipelekwa katika hifadhi ya maiti ya City .