‘Spoil your man this Valentine’s Day’ Julie Gichuru awashauri wanawake

Ikiwa imesalia masaa  mchahe ili siku ya wapendanao ifike aliyekuwa mwanahabari gwiji wa runinga ya Citizen Julie Gichuri amewashauri wanawake wawanunulie wapenzi wao maua na hata kuwafurahisha bali wasitegemee wanaume pekee wawafurahishe.

Valentines ni siku ambayo ilitengwa enzi zile na bado inazidi kuadhimishwa na wengi nchini Kenya, ni siku ambayo inafahamika kama siku ya wapendanao.

Wanawake wengi siku hiyo wanangoja wapenzi wao wawanunulie zawadi tofauti tofauti huku maua yakiwa kipaumbele katika siku hiyo.

Kulingana na Julie kama mwanaume hana pesa na mwanamke ambaye ako naye anahitaji pesa na matumizi mengi anapaswa kutafuta mwanamke ambaye anaelewa vyema kama ana pesa ama hana pesa.

Kupitia mtandao wa kijamii Julie aliandika ujumbe ufuatao;

"To my daughters,

There is nothing more empowering than deciding to break the mold and take control. Get him a rose. Give him a gift. Take the drivers seat and spoil him if you can. A woman must know that she needs nothing from any external forces other than God. She must know that she can handle her business. She therefore needs no man but is able to choose her partner - her homie/lover/friend. That is powerful. Be that woman ♥️ Be different.

Do it your way.

No pressure.

Hii mwaka haitaki makasiriko." Aliandika Julie.

Lakini swali kuu ni je ni wangapi watakao wanunulia waume wao zawadi siku ya wapendanao 14/02/2020 ili kuonyesha upendo wao kwao.