Hata hivyo wanaowatamani hawana bahati kwa sababu wanaume hawa wote wameshachukuliwa, maanake waume hawa wana wapenzi isipokuwa Chimano.
Katika shamra shamra za muziki wao, mabinti wengi walikuwa wanarusha nguo zao za ndani kwenye jukwa huku wakipiga kelele na kusema jinsi wanavyowapenda wanaume hawa.
Wanamziki hawa, ikiwemo Bien walifunguka waziwazi na kuwachumbia wapenzi wao.
Bien alimchumbia mke wake Chiki mbele ya halaiki ya watu.
Savara, ajulikanaye sana kama Mudigi na mashabiki wake, ana mpenzi pia jina lake Yvonne Endo.
Mabinti hawa hujiburudisha na kufanya mambo mengi pamoja kwa sababu waume wao ni wanamziki na marafiki wa chanda na pete.
Zaidi ya hayo, vidosho hawa huitana malkia na mara ya mwisho wapiga picha wa Radio Jambo waliwaona ni wakati wa sherehe ya Oktobafest
Tazama picha ya warembo hawa;