Tommy afunguka mengi kuhusu Msupa S

A0
A0
Msupa S ni mojawapo ya wasanii wa wanawake ambao wanafanya muziki wa kuchana hapa nchini. Ngoma na ambayo alishirikishwa na Khaligraph jones  ilimfanya akavuma zaidi na kujulikana kama mwanadada anayeweza kufanya vizuri zaidi katika tasnia ya sanaa.

Alikutana na mpenzi wake Tommy miaka michache iliyopita. Katika mahojiano na kituo cha utangazaji Tommy amemsifia sana kwa kusema mpenzi wake halewi na ni mwanamke ambaye anaweza aminika.

“Msupa S ni mtu jasiri na mwenye mapenzi  tele na ambaye anaweza songa mbali kimuziki.”

Kando na kuwa mpenzi wake pia ni producer wake. Producer Tommy amesema kuwa mahaba yao huwa sio kisiki katika kazi ya sanaa .

”Tukienda events huwa ni kazi, hatunywi pombe tunafocus sana katika muziki.”

Hali kadhalika aliweza kufunguka jinsi walivyokutana na rapa huyu.

“Nilikutana na Msupa S akifanya muziki wenye asili ya kikalenjin halafu  nikaanza kufanya naye kazi .”