Miaka 37 iliyopita maneja chipukizi katika kampuni ya mashamba ya chai ya Highlands huko Kericho alimwona msichana mdogo mrembo ambaye wakati huo alikuwa chuoni . Kumtazama kwa mara ya kwanza kulikuwa hatua moja ya safari iliyoanza na urafiki kisha hatimaye kumwoa .Edwin Abonyo, mumewe marehemu gavana wa Bomet Joyce Laboso alhamisi alitoa simulizi ya kumbukumbu ya jinsi yeye na Joyce walivyokabiliana na vizuizi katika Uhusiano wao alipojaribu kuishawishi familia ya Joyce kumruhusu kumchumbia binti yao ili baadaye aweze kumwoa .
Na kama ilivyotajiwa babake Joyce Fredrick Laboso alikuwa mkali sana na hakutaka kusikia lolote kuhusu uhusiano wa bintiye na Abonyo . Abonyo amesema alipokuwa akitaka kuzungumza na Joyce Kupitia simu ,binamu yake Sam Ngondi ndiye aliyekuwa akipiga simu kwanza kisha Abonyo angeanza kuzungumza tu baada ya kuthibitisha kwamba sauti katika upande wa pili ilikuwa ya Joyce . Marehemu Laboso atazikwa siku ya jumamosi katika eneo la Koru ,kaunti ya Kisumu .