Mkutano huo unafanyika siku moja kabla ya waakilishi wa kaunti ya jiji kufanya uchaguzi wa kumteua spika mpya baada ya Beatrice Elachi kujizulu siku ya jumanne .
Katika barua kwa kiranja wa wengi katika bunge hilo ,katibu mkuu Raphael Tuju amemtaka Paul Kados kuhakikisha kwamba viongozi wote wa chama hicho wanahudhuria mkutano wa leo .
Wakati huo huo waakilishi wanane wa Jubilee watafika mbele ya kamati ya nidhamu inayoongozwa na Tuju kabla ya mkutano wa leo kuanza . siku ya Jumanne mwenyekiti wa kitaifa wa Jubilee Nelson Dzuya, na waakilishi hao walitakiwa kufika mbele ya kamati hiyo ya nidhamu saa nne asubuhi .
Waliotakiwa kufika mbele ya kamati hiyo ni pamoja na ;John Kamangu Nyumu (Ruai), Millicent Mugambi (Ziwani) Jeremiah Karani (Kayole Central Ward) na Charles Thuo (Dandora Three MCA) wengine ni June Ndegwa, Joyce Kamau, Susan Makungu na Margaret Mbote.