Uhuru aomboleza kifo cha Henry Masaku Ngei

Rais  Uhuru Kenyatta ametuma risala za rambi rambi   kuifariji familia ya  Henry Masaku Ngei aliyefariki  kwa sababu ya saratani ya korodani siku ya jumatano usisku

Ngei,  mwenye umri wa miaka 74,  ni mwanawe wa kwanza  wa mpiganiaji wa uhuru na mbunge wa zamani wa kangundo  Paul Joseph  Ngei

Katika ujumbe wake  kwa familia  ya Ngei  Uhuru alimtaja mwendazake kama mfantyibiashara na mzalendo ambaye alifanya kazi kwa bidii kulistawisha taifa .

" kifo chake kimeinyim akenya mtu ambaye biashara zake katika sekta ya  utalii na kilimo iliwapa maelfu ya wakenya nafasi za kazi’ Uhuru amesema

" katika maisha yake yote Ngei alichangia umoja wa mafanikio ya nchi na ushauri wke wenye busara utakosekana’

Hadi kifo chake  Ngei alikuwa akiendsha hoteli ya  Tala Motel  katika mji wa Tala  na alikuwa mkulima katika eneo la  Kangundo ,Machakos .