Muigizaji Catherine Kamau maarufu kama Kate Actress amekuwa akipinga sana jitihada za kujirejeshea makali ya kiurembo hasa baada ya kujifungua Disemba mwaka jana .
Lakini Kate ana muonekano wa kipekee! Anapendeza kweli na picha zake anazotundika kwenye mitandao ya kijamii zinawaacha wengi vinjwa wazi huku walio na jicho wakijiuliza kama kweli alipata mtoto. Kate ana bahati kweli kwa sababu baada ya kupata mtoto wa kike, mumewe Phil Karanja alimnunulia bonge la zawadi-gari jipya na safi la BMW X1.
Yote hayo kwa sababu tu ya kujifungua mtoto..dah mambo hayo kweli ! Picha za Kate kwenye ukurasa wake zina mvuto wa kipekee na kidosho huyo anapendeza..Zitazame baadhi yazo…