Wakenya 3 ni miongoni mwa waliouawa na Al shabaab Kismayu

Wakenya 3 Miongoni mwa waliouwa na Al shabaab Kismayu 

Wakenya watatu ni miongoni mwa watu 26 waliouwa katika shambulizi la kigaidi katika hoteli moja huko kismayu nchini  Somalia . Rais wa jimbo la Jubaland Ahmed Madobe amesema shambulizi hilo pia liliwajeruhi watu 56  .Tanzania pia imewapoteza raia wake watatu .wengine ni raia wawili wa amerika  ,moja wa Canada na muingereza mmoja .

Mkusanyiko wa Habari na matukio muhimu ..

Mmarekani mbakaji akamatwa

Waendesha mashtaka nchini marekani wame mkamata mwanamme mmoja kutoka jimbo la Pennsylvania  kwa kuwadhulumu kimapenzi wasichana wanne wadogo  katika makaazi ya kuwalinda watoto katika kaunti ya bomet . mshukiwa  Gregory Dow mwenye umri wa miaka 60  alitekeleza dhulma hizo katika makaazi alioznsiaha kuwapa hifadhi watoto mwaka wa 2017 .Atafikishwa kortini Ijumaa wiki ijayo .

Wakimbizi wazuia jitihada za  Kenya kuangamiza Polio

Kenya inaweza kuangamiza kabisa polio endapo itafuata ratiba ya chanjo dhidi ya virusi vya ugonjwa huo .Mtaalam wa matibabu Fredrick Kairithia  hata hivyo anasema kuingia nchini kwa wakimbizi ambao nchi zao hazina mipango ya chanjo kunafanya kuwa vigumu kenya kuafikia hilo .

Waiguru afunga ndoa na kipenzi Waiganjo 

Gavana wa Kirinyaga Anne Waiguru  jana  alifunga ndoa ya kitamaduni na  mpenziwe  wakili kamotho waiganjo . Harusi hiyo ilifanyika katika  shule ya msingi ya  Kiamugumo  kwenye hafla iliyohudhuriwa  na rais uhuru Kenyatta na kiongozi wa  ODM Raila Odinga .

Wakaazi 3000 Magarini waachwa bila makao

 ZAidi ya wakaazi 3000 wa Kadzuhoni  katika eneo bunge la magarini wameachwa bila makao  baada ya nyumba zao kubomolewa na mstawishaji wa kibinafsi . mbunge wa eneo hilo Michael Kingi  amesema ingawaje korti ilikuwa imetoa agizo la kumpa ruhusa msatawishaji huyo ruhusua ya kuwaondoa wakaazi kutoka shamba hilo,wenyeji hao walikuwa tayari wamekata rufaa dhidi ya uamuzi huo na kesi hiyo  ingesikizwa  tarehe 22 mwezi huu .

 Jamaa aliyemuua jirani yake akamatwa 

Polisi huko Kericho  wanamzuilia mshukiwa mwenye umri wa miaka 25  anayedaiwa  kumwua jirani yake kwa kumkata kichwa  na kuwajeruhi watu wengine wawili sieku ya ijumaa usiku . Mshukiwa  Denis Korir  alikamatw akatika kituo cha kibiashara cha Sossiot akitoroka .

Utalii utaimarika mwaka huu 

 Sekta ya  utalii inataraji kuboreka kwa  shughuli za  utalii mwaka huu kuliko ilivyokuwa mwaka jana . maneja mkurugenzi wa  HOteli ya Diani Reef Bobby Kimani  amesema ingawaje kuna upungufu wa asilimia moja  wa idadi ya watalii wanaowasili nchini ,kuna  uwezekano wa idadi hiyo kuongezeka kwa ajili ya kuwepo kwa mashrika mengi ya kufanikisha safari za utalii kutumia mtandao .

 Mwanahabari mashuhuri Somalia Miongoni mwa waliouawa jana

 Takriban watu 26 akiwemo mwanahabari mashuhuri wa Somalia na raia kadhaa wa kigeni wameuawa katika shambulizi la kigaidi lililotekelezwa katika hoteli moja mjini kismayu   kusini mwa Somalia . mlipujia wa kujitoa mhanga alilielekeza gari lililojaa vilipuzi katika hoteli hiyo na kisha baadaye wapiganaji waliojihami kuanza kuwafyatulia watu risasi katika hoteli hiyo .mwanahabari Hodan Nalayeh  mwenye umri wa miaka 43 na mumewe Farid  ni miongoni mwa waliouwa . wakenya watatu pia waliaga dunia katika shambulizi hilo.

Msipeleke mzozo wa ugavi wa mapato kortini,Ruto awaambia magavana

 NAIBU  wa rais William Ruto amewahimiza magavana na maseneta kutowasilisha mzozo wa ugavi wa mapato kortini na badala yake kujadiliana na serikali  na bunge kumaliza utata huo . Wito wake huo unajiri wakati  magavana na maseneta wanapojitayarisha kufanya maandamano kesho hadi bungeni ili kulalamikia utata kuhusu mswada wa ugavi wa mapato unaochelewesha kutolewa kwa pesa za kaunti .

 Team Wanjiku  Mombasa

Gavana wa Nairobi Mike Sonko ataongoza kundi la Team wanjiku kwa mkutano wa hadhara huko Mombasa . Mkutano huo utafanyika katika uwanja wa Aldina katika eneo bunge la  Jomvu. Mbunge wa gatundu kusini moses kuria ,mbunge EALA Simon  Mbungua ,wabunge wa zamani kalembe ndil na Reuben Ndolo pia watahudhuria mkutano huo.

Joyce Akinyi akamatwa na Heroine

Mfanyibiashara Joyce Akinyi alikamatwa jana na Polisi mtaani Nairobi west akiwa  na kilo mbili za heroine .  Akinyi alikamatwa pamoja na raia mmoja wa Congo na watafikishwa kortini hapo kesho .

 Walimu wanafaa kupandishwa vyeo mara moja-knut

 Muungano wa walimu Knut sasa unataka walimu elfu 50 kupandishwa vyeo mara moja baada ya uamuzi wa mahakama  wa siku ya ijumaa ambao unaitaka tume ya TSC kutumia  utaratibu mpya wa kuwahamisha na kuwapandisha vyeo walimu ili kuendeleza pia taaluma zao . Katibu mkuu Wilson Sossion amesema TSC inafaa kujadiliana  kwa haraka na bunge ili kutengewa fedha za kuwapandisha vyeo walimu hao.