Wizara ya afya yaendesha shughuli ya kuwapima wakenya Utawala

EYnfvRUXsAEGIOq
EYnfvRUXsAEGIOq
Kutokana na hatua ya visa vya watu wanaopatikana na ugonjwa wa corona nchini kuendelea kuongezeka kila uchao, wizara ya afya hii leo imeanzisha mchakato wa kuwapima wakaazi wa mitaa ya Utawala, Embakasi Mashariki ili kubaini idadi ya wakenya ambao wanaweza kuwa wameambukizwa virusi hivyo hatari.

Jana waziri Kagwe alisema kuwa serikali imeimarisha viwango vya kuwapima wananchi kwa sailimia 40 baada ya kupokea vifaa bora.

Alisikitikia hatua ya wakenya kukosa kujitokeza kupimwa katika maeneo ambayo serikali ilikuwa imetenga vituo akisema ni vyema kila mtu achukue hatua ili kubaini hali yake ya afya.

Kufikia sasa, Kenya imesajili visa 1,161 vya maambukizi huku idadi ya watu walioaga dunia ikisalia 50