Zaeni Muijaze Tanzania ! Magufuli awashauri wanawake wa TZ

Rais wa Tanzania John Magufuli amewashauri wanawake wa Tanzania kuacha wazi uzazi wao na kuzaa watoto zaidi ili kuboresha uchumi  wan chi hiyo ,ushauri ambao  wakosoaji wanasema  utazidisha hali ya umaskini .“ Mnapokuwa na idadi ya juu ya watu ,inakuwa rahisi kuboresha uchumi . hii ndio kwa sababu uchumi wa China ni mkubwa sana’ amesema Magufuli akitoa mifano ya nchi za India na Nigeria kama baadhi ya mataifa yalio na uchumi thabiti kwa ajili ya idadi kubwa ya watu .

“ Najua wale ambao wamefunga uzazi wao watanilaani  sana kwa matamshi yangu .Jiachilieni  wao wakitaka wajizuie kuzaa’ .Rais Magufuli  aliuambia mkusanyiko wa wenyeji katika mji wa nyumbani kwake wa Chato. Tangu alipochukua maamlaka mwaka wa 2015  alichukua hatua madhubuti ya kuanzisha kampeii ya kuzidisha viwanda chini humo hatua ambayo imesaidia uchumi kuimarika kwa jumla ya asilimia 6-7  kwa  mwaka .

Lakini ameshikilia kwamba ongezeko la idadi ya watanzania litasidia kupiga jeki uboreshaji wa uchumi wa taifa hilo  la afrika mashariki . Tanznia inayokadiriwa kuwa na watu milioni 55 tayari imetajwa kuwa miongoni mwa nchi zenye ongezeko la watoto wanaozaliwa  huku kila mwanamke akikadiriwa kuwa na takriban watoto watano.