Bintiye Raila Odinga Rosemary arejea katika mitandao ya kijamii baada ya kimya cha miaka 4

Rosemary Odinga ameyaptia magumu lakini sasa kuna tabasamu katika nyusoza wengi waliomjua baada ya kuweza kurejhesha uwezo wake wa kuona  .

Bintoye huyo wa kiongozi wa ODM Raila Odinga  ameanza kurejelea maisha ya  kawaida na amechapisha msururu wa picha zake akiwa katika sehemu mbali mbali katika   maisha ya kawaida baada ya kukimya katika mitandao ya kijamii kwa miaka minne . Mama huyo ya watoto wawili  aliweka picha katika instagram huku moja ikiwa  na ujumbe

“stronger than ever.”

Baadhi ya maoni katika posti hiyo iliwoanyesha wengi wanaomshabikia wakiwa na furaka kujua kwamba Rosemary amerejea kwa njia thabiti

carolradull Oh my baby

mongsderr Long time no see

miss.amolo Love the tee

judy_onserio I thank God for your health

evancewashingtonejuma That’s the Spirit my good friend. Always here for you.

Picha yake ya mwisho alioiweka instagram ilikuwa yake na Jalang’o mwaka wa 2016 Novemba  muda mfupi kabla ya kuanza matibabu baada ya kupofuka . Tatizo lake la macho lilianza mwaka wa 2017  alipozirai muda mfupi baada ya kuhutubia mkutano wa mafunzo ya wanawake  kisha akakimbizwa hospitalini kwa ambulansi .

Baadaye alisimulia jinsi alivyokuwa na maumivu makali ya kichwa  lakini akapuuza ,baadaye alipatikana kuwa na uvimbe katika ubongo wake na hata akajipata katik coma . Baadaye kaika mahojiano babake Raila alisimulia jinsi kundi la madaktari 10 wa China walivyoweza kuokoa maisha yake katika upasuaji uliodumu kwa saa 10 katika chuo kikuu cha  Peking .

Waziri huyo mkuu wa zamani amesema maisha ya binti yake yaliokolewa China baada ya miezi mitatu ya matibabu afrika kusini na Israel bila mafanikio.Odinga  pia amefichua kwamba Rosemary alianza kuona baada ya kutumia matibabu ya dawa za kiasili kutoka India .