Bunge litapiga kura leo kufanyia marekebisho sheria ya malipo ya uzeeni ili kuwapa wabunge hao wa zamani pensheni watakayolipwa kila mwezi maisha yao yote .
Marekebisho hayo yaliofanywa kwa sheria ya malipo ya uzeeni kwa wabunge yatapitishwa kwa urahisi bungeni .pensheni hiyo ya kila mwezi itaongezwa kutoka shiingi 2000 kwa sasa hadi shilingi 125,000 kila mwezi .
Malipo ya fedha hizo huenda yakarejeshwa nyuma hadi julai mwaka wa 2010 hatua ambayo huenda ikailazimu serikali kutoa mamilioni ya pesa kutekeleza pensheni hiyo .
Iwapo rais Uhuru Kenyatta ataidhinisha msswada huo kuwa sheria wabunge 290 huenda wakaanza kulipwa kiasi cha chini ya shilingi 100,000 kama pensheni kila mwezi
Ofisi ya bajeti bungeni imeashiria kwamba serikali huenda ikawalipa wabunge hao wa zamani shilingi milioni 15.1 kila mwezi .