Mamake Sandra na dadake Esma huenda ndio kikwazo kikubwa kwa mwanamuziki huyo kudumu katika mahusiano na wanawake wengi ambao amewahi kuhusishwa nao na hata kuzaa nao watoto .
Nyota huyo ametoa wimbo kwa jina Haunisumbui, unaoonekana kuw ana ujumbe foche kuwalenga Hamisa Mobetto na Tanasha
Unasema hivi wimbo huo ;
Si ko ko si kanda mbili yani vyote
Haviku pendezi kuwa na ngoko
Usio nawiri tope niutelei
Utaishia kututabiri
Tubomoke ina songa miezi
Mola amesha taka dhiri usijichoshe
Haivunjiki penzi
Hazikukai mascara wala makeup zina kushuka uso ume ku parara
Zingetenguka uso sauti yastara kwa kudeka
Una weuke jibwa koko la mbagala
ina bweka na kubwetuka wala
Wala hunisumbui wala
Wengi wamelitafisiri hilo kama kijembe cha moja kwa moja kwa wapenzi wake hao wa zamani kwa tabia zao. Dadake Diamond Esma aliutuma wimbo huo na maneno haya;
TOBA TOBAAA SASA MAEX ZETU SI WATATUCHAMBA TUKOME TUITWE KUNGURU NA MAKEUP ZETU ZA KUTUSHUKA NA USO UMETUPARARA… ALAFU KUTWA KWA MAPAGE FAKE KM @JUMALOKOLE2
Mamake alijibu kwa kusema
HAIYA WALE WATEGEMEA MAKEUP OOOYOOOOO.
Watumizi wa mitandao ya kijamii nao hawakunyamaza na majibu yao kwa drama hiyo ilikuwa kama hivi ;
samlucksamadizo Hiii familia kweli mediocres
mamak_eshania Mediocres yaani kumbe pia wanaume hujua kuchamba waaah… This is new… Unachamba mwanamke umewaijifunika naye blanket and you think karma itakuspare
witnessjustus Tabu ya kudate na waswahil utaimbiwa taarabu paka bas pole kwa ma X wote wa huyo mtandale