Hatukulala pamoja-Carol

Hakuna kilichofanyika kati yangu na Eric Omondi tukiwa ‘honeymoon’- asema Carol

“ Hakuna kilichofanyika na iwapo ningepata mimba ya ERIC BASI NITAIHIFADHI ..LAKINI SASA HAKUNA WATOTO .

Muhtasari
  •  Carol ambaye alimaliza kama mshindi ili  kuwa  ‘mke’ wa Omondi  amekana  kuwa alishiriki mapenzi na Eric Omondi  wakati  wakiwa katika ‘ honey moon’  huko pwani
  •  Watu wengi hawaamini kwamba hakuna kilihofanyika katika siku moja au mbili ambazo Omondi na  Carol walikuwa pwani
Eric na Carol

Waimbaji wa kundi la BandBeca Carol na  Becky  waligonga vichwa vya Habari kwa kushiriki katika kipindi cha  maigizi cha  Eric Omondi ,Wife material

 Carol ambaye alimaliza kama mshindi ili  kuwa  ‘mke’ wa Omondi  amekana  kuwa alishiriki mapenzi na Eric Omondi  wakati  wakiwa katika ‘ honey moon’  huko pwani

 Watu wengi hawaamini kwamba hakuna kilihofanyika katika siku moja au mbili ambazo Omondi na  Carol walikuwa pwani . Carol akizungumza katika kipindi cha Ilikuaje  cha Maqssawe Japani katika radio Jambo hata hivyo amesema yote yalikuwa maigizo na kwamba alihusika katika kipindi hicho ili kutangaza album yao ya muziki .

 “ Hatukulala katika chumba kimoja  ,iwapo hicho ndicho unachouliza .kila mtu alikuwa katika chumba chake

 Sababu ya watu wengi kutoamini kauli ya Carol ni kwamba palitokea picha nyingi ambazo walipiga katika sehemu mbali mbali zikiwemo katika bafu … huku katika picha nyingine wakionekana kukumbatiana na wakipapasana .

 “ Hakuna kilichofanyika na iwapo ningepata mimba ya ERIC BASI NITAIHIFADHI ..LAKINI SASA HAKUNA WATOTO .