Hii valentines nitacheza kama mimi,'Kabi wa Jesus amwambia mkewe huku akifichua alama alizopata KCSE

Muhtasari
  • Kabi afichua hakupata alama ya D+ katika mtihani wake wa KCSE
  • Pia alisema kwamba atacheza kama yeye siku ya wapendanao kwa maana mkewe alifanya maajabu mwaka jana siku yake ya kuzaliwa
Kabi wa jesus
Kabi wa jesus

Familia ya Kabi Wa Jesus iafahamika sana kwenye mitandao ya kijamii kwa kutafuta kiki na kuishi maisha ambayo si yao kulingana na mashabiki wengi.

Mwaka jana bibi yake Kabi alimpa zawadi za kipekee wakati wa kusheherekea siku yake ya kuzaliwa.

Kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram alipakia picha za siku hiyo huku akiahidi mkewe kuwa siku ya wapendanao pia naye atacheza mchezo wake.

 

Moja ya bora zaidi #Tbt ill. @millywajesus wewe ni wa baraka katika maisha yangu.Manze nakupenda saaaaaana 🥰🥰🥰 pia mimi lazima nicheze kama mimi this valentines 💝."

kabi
kabi

Pia kupitia kwenye mitandao yake ya youtube alifichua kwaba alifanyia mtihani wake akiwa jela.

Kabi alisema kwamba hakupata alama ya D+ kama vile uvumi umekuwa ukisema bali alipata alama ya C+ kwa maana yeye sio mjinga kiasi kile.

"Sikupata alama ya D+ nakaa hivyo mjinga?nilipata alama ya C+," Alisema Kabi.