Kanye West abadilisha jina lake kuwa Ye

Jina lake la awali- Kanye Omari West - halitatumika tena.

Muhtasari

•Jaji wa Los Angeles aliridhia ombi la rappa huyo kubadilisha jina, afisa mawasiliano katika Mahakama Kuu ya Los Angeles alithibitisha.

•Rapa huyo, anayejulikana sana kwa vibao kama vile Gold Digger na Stronger, alikua akitumia Ye kama jina la utani na mnamo 2018 alilitumia kama jina la albamu.

Image: GETTY IMAGES

Msanii wa Marekani aliyekua akijulikana kama Kanye West sasa itajulikana rasmi kama wewe tu.

Jaji wa Los Angeles aliridhia ombi la rappa huyo kubadilisha jina, afisa mawasiliano katika Mahakama Kuu ya Los Angeles alithibitisha.

Nyota huyo wa miaka 44-aliwasilisha ombi hilo mwezi Agosti, akitoa "sababu za kibinafsi."

Rapa huyo, anayejulikana sana kwa vibao kama vile Gold Digger na Stronger, alikua akitumia Ye kama jina la utani na mnamo 2018 alilitumia kama jina la albamu.

Muda mfupi baada ya kutolewa kwa albamu hiyo, alitweet: "Kujulikana rasmi kama Kanye West. Mimi ni YE."

Sasa amelifanya rasmi na jina lake la awali- Kanye Omari West - halitatumika tena.

Ijapokua jina la Ye tayari lilikua likitumia kwenye Twitter, akaunti yake ya Instagram na wavuti yake bado inatumia jina lake la zamani kufikia Jumanne.

"Ninaamini 'Ye' ni neno linalotumiwa sana katika Biblia, na katika Biblia linamaanisha wewe. Kwa hivyo mimi ni wewe, mimi ni nyinyi, yaani ni sisi," alisema katika mahojiano ya 2018 na mtangazaji wa redio Big Boy.

Wasnii wengine waliobadilisha jina ni Prince, Snoop Dogg na Sean Love Combs, wengine wao mara kadhaa.