• Juma Lokole amejitokeza wazi na kutetea Salam baada ya kuonekana na mpenzi wa zamani wa Harmonize, Sarah kwenye eneo la Burudani.
• Alikanusha madai kwamba Salam na Sarah wako kwenye mahusiano huku akisema aliyeanzisha mazungumzo alikuwa Sarah wala si Salam kama watu wanavyosema.
Mwandani wa Diamond,Juma Lokole amejitokeza wazi na kutetea Salam baada ya kuonekana na mpenzi wa zamani wa Harmonize, Sarah kwenye eneo la Burudani.
Hivi majuzi kumekuwa na habari zikienea hasa kwenye mitandao ya kijamii kwamba Sarah amekuwa katika mahusiano ya siri na mmoja wa wanachama wa lebo ya Wasafi.
Lokole kupitia kipindi kimoja nchini Tanzania alikanusha madai kwamba Salam na Sarah wako kwenye mahusiano huku akisema aliyeanzisha mazungumzo alikuwa Sarah wala si Salam kama watu wanavyosema.
"kwanza acha niliweke jambo hili kuhusu Salam na Sarah, wale walikutana Zanzibar...Salam alikuwa kwenye mambo yake ya kukaribisha mwaka mpya na Sarah alikuwa kwenye mambo yake tunajua alikuja Tanzania na tulimuona juzi aliposti, walikutana si kwa ubaya lakini walikuwa hawaongei...Sarah ndiye alimsalimu wa kwanza Salim. Huwa anamuita meneja... kama walitembea pamoja basi.. .walitembea pamoja kwa sababu ya akili ya pombe' alisema Juma Lokole."
Aliendelea kusema sababu ya mpenzi huyo wa zamani wa Harmonize kurejea nchini Tanzania ili kufuatilia mali zake.