Amber Ray atafuta mwanamume wa Kumchumbia

Muhtasari

• Amekiri anatafuta mwanaume wa kuchumbiana naye mwaka huu 2022

• Alieleza kuwa haoni kama kuna mwanamume aliyechumbiana naye mwaka jana atakaemchumbia mwaka huu.

• Isitoshe aliwatania wapenzi wake wa zamani kwa kuwambia waende kuchukua vyeti vyao kwani vishatoka.

Amber Ray
Image: Hisani

Sosholaiti Amber Ray amekiri anatafuta mwanamume wa kuchumbiana naye mwaka huu 2022.

Kupitia ukurusa wake wa  instagram, alieleza kuwa haoni kama kuna mwanamume aliyechumbiana naye  mwaka jana atakuwa naye mwaka huu.

Mama huyo wa  mtoto  mmoja aliwataarifu wanaume wapya wanaomtamani na wako tayari  kumchumbia waanze kutuma maombi yao haraka iwezekanavyo kabla nafasi kufungwa.

Isitoshe aliwatania wapenzi wake wa zamani kwa kuwambia waende kuchukua vyeti vyao kwani viko tayari.

"Wale niliotoka nao mwaka 2021 vyeti vyao  vimetoka, tafadhali njoo uchukue na 2022  uandikishaji  wa wapenzi wapya unaendelea, ingawa nafasi ziko finye."

Amber Ray alifunga ndoa  na mmiliki wa Matatu, Jimal Rohosafi lakini ikadaiwa  wapenzi hao waliachana kwa madai kwamba mume wake alikuwa na mpango wa kando.