Pasta Ng'ang'a awaunganisha vijana single madhabahuni, kila mmoja ajichagulia wa kwake (video)

“Sisi watu wa Mungu hatuwezi kaa na watu hapa na wana spiritual gap. Tufanye ibada kwa ajili ya hawa watu” Aliomba mkutano wa waumini katika kanisa lake.

Muhtasari

• “Aaa uuuwi! Kwani hii kanisa ni ya ma-singles tu?” Kiongozi wa dini alishtuka akiwa kwenye mimbari.

• Pasta Ng’ang’a aliomba waumini wa ibada hiyo kuwafanyia maombi maalum ili waweze kuoa na kuolewa pia.

Pasta Ng'ang'a.
Pasta Ng'ang'a.
Image: Screengrab

Mchungaji James Maina Ng’ang’a amefanya jamo la kiajabu kabisa katika kanisa lake baada ya kufanya jaribio la kuwaunganisha wanaume single na warembo single kwenye madhabahu.

Katika video ambayo inaenea katika mitandao ya kijamii, Nga’ng’a aliwaita wanaume ambao hawana wapenzi kujongea katika madhabahu ya kanisa lake la Neno Evangelism.

“Wale wanaume hamjaoa simama. Wenye hamna mke kwa nyumba,” Aliwaita wanaume kwenye mimbari.

Bila kutarajiwa kwake, wanaume walimiminika kwenye mimbari na kumfanya mwinjilisti wa televisheni ashtuke.

Kulingana na mhubiri huyo, hakuwahi kufikiria kuwa kanisa lake lingeweza kuzaa kusanyiko la watu wasio na waume kwa njia hiyo.

Baada ya kuona idadi ya wanaume wasio na wapenzi ni nyingi, mchungaji huyo mtata aliwaita warembo wasio na wapenzi pia kujongea jukwaani kujumuika na wenzao wa kiume.

“Aaa uuuwi! Kwani hii kanisa ni ya ma-singles tu?” Kiongozi wa dini alishtuka akiwa kwenye mimbari.

“Ilikuwa nafikiri tuite wale wamama hawajaolewa wasimame hapa waone. Kama kuna nyota ilipotea yako, leo nyota yako inarudi. Nyota iko hapa. Njia imefunguka tunaondokea,” Alisema wakati wanawake wasio na waume wakivamia mimbari.

Kufuatia idadi kubwa ya waamini kwenye madhabahu, kasisi aliwatania wanawake ili kuwaona wanaume ambao wanahisi wanaweza kuendana ingawa wanawake wengi walishindwa kuchukua kazi hiyo.

Pasta Ng’ang’a aliomba waumini wa ibada hiyo kuwafanyia maombi maalum ili waweze kuoa na kuolewa pia.

“Sisi watu wa Mungu hatuwezi kaa na watu hapa na wana spiritual gap. Tufanye ibada kwa ajili ya hawa watu” Aliomba mkutano wa waumini katika kanisa lake.

Hatua ya mhubiri huyo kuandamana kwa watu wasio na waume kwenye mimbari inakuja miezi sita baada ya kutoa makataa ya miezi sita kwa watu wote wasio na waume kuolewa kabla hawajakabiliwa na hasira yake. hasira lakini aliyesalia atalazimika kulikabili shoka lake.