โข Bahati walisema ni ishara ya mapenzi wengine wakipinga kwa kauli kwamba huo ni ukichaa katika mapenzi.
Wakuza maudhui Diana Marua na Kevin Bahati wamewaacha mashabiki na watumizi wa mtandao wa Instagram katika hali ya mshangao baada ya kupakia video wakishiriki kupiga mswaki kwa kutumia mswaki mmoja.
Wawili hao walionekana katika hali ya furaha huku kila mmoja akiuchukua mswaki huo huo mmoja kwa zamu kutoka kwa mdomo wa mwenzake.
Baadae hata kabla ya kusukutua, Diana alionekana akitaka kumbusu Bahati kabla ya wote kucheka.
Waliandika;
โYako ni Yangu; Yangu ni Yako โค๏ธ Nitangโa Ngโana Nawe ๐๐๐๐๐๐๐.โ
Hatua hii ya kubadilishana mswaki kutoka kwa mdomo wa Bahati kwenda kwa mdomo wa Diana na kurudia ilivutia maoni tofauti kutoka kwa mashabiki wao.
Bahati walisema ni ishara ya mapenzi wengine wakipinga kwa kauli kwamba huo ni ukichaa katika mapenzi.
โUongo mbaya! Siwezi kushiriki mswaki wangu ๐๐๐ afadhali mninyonge,โ Njambi Fever.
โDiana siuko na bahati ,unaishi kimalaika utaenda Heaven direct,โ Eddy Musomb alisema.
โNikifika hapa mnipige risasi ya figo.โ Sebastian Obk.
โUwiiiii nimehisi kutapikaaโ Zahras Choice alisema.