Ripoti ya uchunguzi wa kifo cha Mohbad yakosa kubaini kilichomuua, miezi saba baadae

Mwanapatholojia alisema mwili ulipaswa kufukuliwa ndani ya saa 12 baada ya kuzikwa ili kuepusha kuoza. Kwa hiyo mukhtasari anaousema ni kwamba sababu ya kifo haiwezi kufahamika," alisema.

Moh Bad
Moh Bad
Image: Instagram

Jumatano alasiri nchini Nigeria, kulishuhudiwa na Hasira kutoka kwa watumiaji wa mtandao kwani baada ya kusubiri matokeo ya uchunguzi wa maiti ya Mohbad kwa zaidi ya miezi 7, na ripoti kuwekwa wazi ikishindwa kubaini chanzo cha kifo chake.

Kumbuka kwamba mwimbaji huyo alikufa chini ya hali ya kutiliwa shaka sana baada ya onyesho la mwaka jana.

Kwa mujibu wa chombo kimoja cha habari nchini humo, Mwanasayansi wa Uchunguzi wa maiti kutoka Hospitali ya Taaluma ya Chuo Kikuu cha Jimbo la Lagos (LASUTH), Prof. Sunday Osiyemi amewambia wachunguzi wa kifo cha Mohbad kwamba matokeo ya uchunguzi wa maiti uliofanyika mwili wa marehemu umeshindwa kufahamu chanzo cha kifo hicho.

Prof.Osiyemi alimweleza mchunguzi wa kifo hicho, Hakimu Adedayo Shotobi kuwa hitimisho hilo linaweza kuchangiwa na sababu kadhaa, mojawapo ikiwa ni kwamba ilichukua muda mrefu, takribani siku 21 kabla ya kufanyika kwa uchunguzi huo ambao mwili huo ulikuwa umeoza na kuzikwa.

Akitoa ufafanuzi zaidi juu ya shauri hilo, wakili wa familia ya Mohbad, Wakili Mwandamizi wa Nigeria, Wahab Shittu alisema, “Mwanapatholojia alisema mwili ulipaswa kufukuliwa ndani ya saa 12 baada ya kuzikwa ili kuepusha kuoza. Kwa hiyo mukhtasari anaousema ni kwamba sababu ya kifo haiwezi kufahamika na unaposema sababu ya kifo haiwezi kufahamika, maana yake ni tuhuma, haiko wazi, hakuna sababu maalum.”

Wakili huyo pia alisema mwanapatholojia alirejelea baadhi ya dawa alizotumiwa marehemu Mohbad kabla hajafariki jambo ambalo lingeweza kusababisha athari ambayo ilifanya iwe vigumu kubaini chanzo cha kifo.

Shittu alisema, "Pia alienda mbali zaidi na kusema kwamba inaweza kuhusishwa na athari za dawa fulani alizopewa kabla ya kufa. Tena basi akafuzu kusema kwamba hajui kama ni dawa hizo ndizo zilizosababisha kifo chake”.

Mchunguzi wa kesi ameahirisha hadi Juni 11 kwa ajili ya uchunguzi wa Mwanapatholojia.