Kwa nini babake Mohbad amekataa kuchukua mwili wa mwanawe kwa ajili ya maziko

"Babake akiandika [barua] leo, bila shaka maiti itatolewa na lazima aibebe maiti. Huwezi kuandika na kuiacha hapo. Kwa nani?”

Muhtasari

• Mamake Mohbad mnamo Jumanne, Novemba 21, 2023 anasema kwamba mwili wa mwimbaji huyo umetolewa kwa baba lakini amekataa uzikwe upya.

Mohbad na babake
Mohbad na babake
Image: Screengrab

Baada ya miezi miwili ya mitazamo tofauti kuhusu kifo cha msanii Mohbad, hatimaye polisi wamekamilisha uchunguzi wa maiti iliyofukuliwa lakini inaarifwa kwamab babake Mohbad amekataa kuuchukua mwili huo kwa ajili ya kumpumzisha mwanawe.

Kwa mujibu wa blogu ya Linda Ikeji ambayo ilizungumza na polisi mmoja aliyetaka jina lake kubanwa, mzee huyo amearifiwa mapema wiki hii kuhusu kuuchukua mwili huo lakini amekataa kwamba hatoweza kuuchukua kwa ajili ya maziko kwa sababu kadhaa.

Mamake Mohbad mnamo Jumanne, Novemba 21, 2023 anasema kwamba mwili wa mwimbaji huyo umetolewa kwa baba lakini amekataa uzikwe upya.

Kwa mujibu wa polisi, baba mzazi ndiye pekee mwenye uwezo wa kukabidhiwa mwili huo pindi tu atakapotuma ombi la kukabidhiwa mwili, lakini mzee amekataa akisisitiza kwamba anataka uchunguzi mwingine wa DNA kufanywa ili kukubali kumzika mwanawe.

“Mwili uko katika chumba cha kuhifadhia maiti. Haijatolewa. Haingeachiliwa kwako na usingekuja na kuichukua. Hospitali haikuruhusu. Baba pekee ndiye anayeweza kuomba maiti hiyo kutolewa, ni baba tu na polisi wamesema siku yoyote akiomba angeipata mara moja. Tumewaambia muda wowote wakitaka waandike tu maombi lakini baba amekataa kufanya hivyo.”

“Kitaalam, ni baba ambaye anajizuia. Baba huyo amesema bado hatachukua hadi wafanye DNA na hilo ni tatizo lao la kifamilia. Babake akiandika [barua] leo, bila shaka maiti itatolewa na lazima aibebe maiti. Huwezi kuandika na kuiacha hapo. Kwa nani?”

Lindaikejiblog on Instagram: "The police in Lagos state has said that they have informed Joseph Aloba, the father of late singer, Ilerioluwa Aloba aka Mohbad, that he can come and collect the corpse of his son anytime he wants but the man has not yet applied for it. Recall that the mother of the singer released a video on Tuesday, November 21, saying that the body of the singer has been released to the father but he has refused for it to be reburied. Findings by LIB showed that the police, having concluded the autopsy on the singer, informed the father that he can come forward to collect his body but the man is yet to apply for it. A police source who spoke to LIB on condition of anonymity, said ‘’The body is in the morgue. It has not been released. It wouldn't be released to you and you wouldn't come and pick it. The hospital wouldn't allow it. Only the father can apply for the release of the corpse, only the father and the police has said any day he applies, he would get it immediately. We have told them, anytime they want it, just write an application but the father has refused to do that. Technically, it is the father that is holding back. The father has said he is not taking it yet until they do DNA and that is their personal family problem. If the man writes today, of course it will be released and he must carry the corpse. You can't write and keep it there. For who?'' Recall that the singer who passed away on September 12, was buried the next day, September 13. Following the controversy surrounding his demise, an autopsy was demanded for by Nigerians and his body was exhumed on September 21. It has not been reburied since then and the autopsy result is yet to be made public. Mr Aloba has repeatedly insisted that a DNA must be done to ascertain the true paternity of Liam, the seven month old son of late Mohbad and his wife, Wunmi."

Kumbuka kwamba mwimbaji huyo aliyeaga dunia Septemba 12, alizikwa siku iliyofuata, Septemba 13. Kufuatia utata wa kifo chake, uchunguzi wa maiti ulitakiwa na Wanigeria na mwili wake ukafukuliwa Septemba 21. Haujazikwa tena tangu wakati huo. na matokeo ya uchunguzi wa maiti bado hayajawekwa wazi.

Bw Aloba – babake - amesisitiza mara kwa mara kwamba lazima DNA ifanywe ili kujua asili ya kweli ya Liam, mtoto wa miezi saba wa marehemu Mohbad na mke wake, Wunmi.