Mkewe Ida Odinga,kakake mkubwa Oburu Odinga na dadake mdogo Ruth Odinga wamesema kwamba Raila hayupo hatarini lakini hatarejea nchini hivi karibuni .
Ida Ida amesema mume wake alitibiwa tatizo la neva lilikuwa likimpa shida katika mguu wake mmoja na anahitaji muda zaidi wa kupumzika . Kwa ajili ya matibabu aliyopokea atasalia UAE hadi atakapoweza kurejelea shughuli za kisiasa .
Familia hiyo imeeleza kufadhaika na habari zinazosambazwa katika mitandao ya kijamii zikieleza maradhi ambayo Raila anadaiwa kuugua .
Ida amesema habari kama hizo zinafaa kupuuzwa na wakenya kama uvumi na amewashukuru wakenya wenye nia njema ambao wamekuwa wakimuombea Raila afueni ya haraka.
Ida alisema bwana Odinga yupo katika hospitali moja inayoendeshwa na wajerumani ,Dubai .
Ilikuwa mara ya kwanza kwa Ida kufunguka kuhusu tatizo la afya la mumewe huku akiongeza kwamba amekuwa akizungumza naye karibu ‘kila saa au baada ya saa mbili’