Kuna maambukizi ya awamu ya pili ya corona

Covid 19: Ufaransa yatangaza kafyu ya usiku kukabiliana na usambaaji wa corona

Nchi nyingi ulaya zimerejesha vikwazo

Muhtasari
  •  Ufaransa yasajili idadi ya juu zaidi ya maambukizi tangu kuanza kwa janga 
  •  Kuna hofu kwamba zuio la kuttoka nje litawekwa katika maeneo mengi 

 

Macron na mkewe Brigitte

 Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron ametangaza marufuku ya kutotoka nje katika  mji wa Paris na miji mingine  nane ili kuzuia usambaaji wa virusi vya corona

 Kafyu hiyo ya kuanzia saa tatu  usiku hadi saa kumi na mbili alfajiri  itaanza kutekelezwa siku ya jumamosi  na kudumu kwa takriban wiki nne  Bwana Macronm ametangaza .

 Hali ya  dharura  ya kiafya pia imetangazwa.

  Kwingineko katika nchi ya Ujerumani serikali imetangaza kufungwa mapema  kwa baa na mikahawa katika maeneo yenye hatari

 Chansela  Angela Merkel  ametangaza vikwazo hivyo siku ya jumatano  wakati taifa hilo liliripoti visa zaidi ya 5000 vya  corona  kwa mara ya kwanza tangu mwezi aprili .

 Siku ya alhamsi  idadi hiyo iliongzeka tena bvaada ya watu 6,638 kupatikana na virusi vya corona  ambayo ndio idadi ya juu Zaidi tangu kuanza kwa janga la corona .

 Chini ya sheria mpya , maeneo ambako maambukizi yatafika asilimia 50 kwa kila idadi ya watu laki moja yanafaa kufunga baa  kufikia saa tano usiku .

  Mikusanyiko ya watu binafsi inafaa kuwahusisha watu kumi pekee kutoka nyumba mbili .

 Kote barani ulaya  serikali za nchi hizo  zimeanza kurejesha mikakati na vikwazo vya hapo awali huku pakizuka awamu ya pili ya maambukizi ya corona .

 Kuna zuio la  kutotoka nje katika baadhi ya sehemu za Uholanzi huku  mikahawa na maeneo ya burudani ikifungwa .