- Jeshi la Uganda lakita kambi nje ya nyumba ya Bobi Wine kabla ya kampeni
Kiongozi wa upinzani nchini Uganda Robert Kyagulanyi, al maarufu Bobi Wine, ametuma picha ya polisi na jeshi wakionekana nje ya nyumba yake kabla ya kampeni za uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika katika wilaya ya Kayunga.
Rais Yoweri Museveni anatarajiwa kutembelea katika wilaya ya Kayunga kumfanyia kampeni mgombea wa chama tawala anayewania nafasi ya uenyekiti.
Uchaguzi huo mdogo umepangwa kufanyika Alhamisi na chama tawala na upinzani kwa pamoja vinataka kuonyesha uwezo wao katika eneo hilo.
Bobi Wine ameshutumu jeshi na polisi kwa kujaribu kumzuwia kuondoka nyumbani kwake :
Vyombo vya habari nchini Uganda vimeripoti kuwa polisi na jeshi pia wamepelekwaKayunga kabla ya kampeni za Jumanne.
#DictatorMuseveni is so shameless. He places me under house arrest, and then uses tax payer's money to ferry people to go see him in Kayunga! This is why we are not giving up until Uganda is free.#WeAreRemovingADictator pic.twitter.com/jENcenKaEm
— BOBI WINE (@HEBobiwine) December 14, 2021
Awali Kayunga ilikuwa ni ngome ya chama tawala hadi mwenyekiti wa zamani aliyefarikiakiwa madarakani alipochaguliwa kutoka upinzani.
Chama tawala kinataka kurejesha tena kiti hicho na kimeahidi kuufanya mji huo kuwa manispaa, imeripoti gazeti la Daily Monitor.