Kiongozi wa jeshi la Burkina Faso akubali kujiuzulu baada ya mapinduzi

Raia wengi nchini Burkina Faso hawajahisi kuwa salama kwa muda.

Muhtasari

•Kiongozi mpya wa nchi hiyo aliyejitangaza, Kapteni Ibrahim Traoré, alilazimisha kujiuzulu kwa Luteni Kanali Paul-Henri Damiba na masharti aliyoweka.

•Burkina Faso imekumbwa na mapinduzi manane tangu uhuru mwaka 1960.

Image: BBC

Kiongozi wa kijeshi wa Burkina Faso, ambaye alitimuliwa katika mapinduzi siku ya Ijumaa, amekubali rasmi kuachia ngazi, viongozi wa kidini na jumuiya walisema.

Walisema kiongozi mpya wa nchi hiyo aliyejitangaza, Kapteni Ibrahim Traoré, alilazimisha kujiuzulu kwa Luteni Kanali Paul-Henri Damiba na masharti aliyoweka.

Tangazo hilo lilifuatia mashambulizi dhidi ya taasisi za Ufaransa, baada ya kuripotiwa kuwa Lt Kanali Damiba alikuwa akihifadhiwa katika kambi ya kijeshi ya Ufaransa. Ni mapinduzi ya pili mwaka huu. Katika visa vyote viwili, hali mbaya ya usalama nchini humo na kushindwa kukabiliana na waasi wa Kiislamu kulilaumiwa kwa unyakuzi huo.

Burkina Faso inadhibiti kidogo kama 60% ya eneo lake, wataalam wanasema, na ghasia za makundi ya kigaidi zinazidi kuwa mbaya.

Umoja wa Afrika umetaka kurejeshwa kwa utaratibu wa kikatiba ifikapo Julai 2023 hivi punde, ukikubaliana na jumuiya ya kikanda ya Jumuiya ya Kiuchumi ya Afrika Magharibi (Ecowas) kwamba kuondolewa madarakani kwa kiongozi Lt Kanali Damiba "kulikuwa kinyume na katiba".

Hapo awali Ecowas ilisema "haikuwa sawa" kwa waasi wa jeshi kunyakua mamlaka wakati nchi hiyo inajitahidi kuelekea utawala wa kiraia. Mapinduzi yaliyoahidi na kushindwa kuleta usalama.

Hakuna taarifa iliyotolewa moja kwa moja na Lt Kanali Damiba. Lakini viongozi wa kidini na jamii walisema Luteni Kanali Damiba mwenyewe alijitolea kujiuzulu "ili kuepusha makabiliano na madhara makubwa ya kibinadamu na mali," kulingana na nukuu zilizotajwa na shirika la habari la AFP.

Walisema Luteni Kanali Damiba aliweka masharti saba ya kuachia ngazi - ikiwa ni pamoja na hakikisho la usalama wake, makubaliano ya kuendelea na juhudi za maridhiano ya kitaifa na kuendelea kuheshimu dhamana ya kurejea kwa utawala wa kiraia ndani ya miaka miwili.

Kanali aliyeng'olewa madarakani alimwondoa mwenyewe madarakani Rais Roch Kaboré mnamo Januari, akisema kwamba ameshindwa kukabiliana na ongezeko la ghasia za wanamgambo wa Kiislamu.

Raia wengi nchini Burkina Faso hawajahisi kuwa salama kwa muda. Uasi wa Kiislamu ulizuka nchini humo mwaka wa 2015, na kusababisha maelfu ya watu kupoteza maisha na kuwalazimisha takriban watu milioni mbili kutoka makwao.

Burkina Faso imekumbwa na mapinduzi manane tangu uhuru mwaka 1960.