Moses Kuria ataka ombi la Raila katika mahakama ya juu kutupiliwa mbali kuhusu machafuko Bomas

Muhtasari
  • Haya, anasema, yalijiri Jumatatu, Agosti 15, wakati Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati alipotazamiwa kutangaza matokeo ya uchaguzi wa urais
Mbunge wa Gatundu Kusini Moses Kuria mnamo Jumatano Machi 30, 2022 alipofika mbele ya IEBC Nairobi.
Mbunge wa Gatundu Kusini Moses Kuria mnamo Jumatano Machi 30, 2022 alipofika mbele ya IEBC Nairobi.
Image: MAKTABA

Aliyekuwa Mbunge wa Gatundu na kiongozi wa chama cha Chama cha Kazi Moses Kuria amehamia Mahakama ya Juu kupinga kiongozi wa muungano wa Azimio La Umoja One Kenya Raila Odinga.

Odinga mwenyewe aliwasilisha ombi Jumatatu akitaka kupinga matokeo ya uchaguzi wa urais wa Agosti 9 kuhusu wasiwasi kwamba utawala wa sheria haukufuatwa katika zoezi hilo ambalo lilimfanya kushindwa na mpinzani wake mkuu, William Ruto.

Katika ombi lake, Kuria ambaye ni mshirika wa Ruto anamshtumu Odinga kwa kutumia ajenti mkuu wa chama chake, Saitabao Ole Kanchory, na wengine kusababisha ghasia katika kituo cha kitaifa cha kujumlisha kura za Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) katika Bomas of Kenya jijini Nairobi.

Haya, anasema, yalijiri Jumatatu, Agosti 15, wakati Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati alipotazamiwa kutangaza matokeo ya uchaguzi wa urais.

Huku akimtaja Odinga na chama cha muungano cha Azimio kuwa wahojiwa wa kwanza na wa pili mtawalia, Kuria anawashutumu maajenti wao kwa kumpiga Bw. Chebukati.

"Raila Odinga kupitia kwa wakala Mkuu Kanchory na wengine walisababisha vurugu katika Kituo cha Kukusanya kura cha Bomas of Kenya, kumvamia kimwili Msimamizi wa Kitaifa wa Uchaguzi na makamishna wengine na hata kuchomoa bunduki.

Raila ataondolewa kwenye Ombi la Mahakama ya Juu kwa kuwa haji na mikono safi. Acha haki itiririke kama kijito kikubwa."