- Angenichagulia nguo ambayo ningevaa nikienda kazini ….wakati mwingine nikijipodoa angesimama kando ya kioo akishangaa mbona najipodoa sana’ anasema Lisa
- Kwa takriban mwezi mmoja alikuwa amenuna na hakuna aliyekuwa akizungumz ana mwingine .
Wakati mwingi pana migogoro kati ya wanandoa kuhusu mwanamke kufanya kazi .Ingawa kuna wanaume ambao hawana tatizo na wake zao kufanya kaiz ,kuna idadi kubwa ya wanaume ambao hupata tatizo sana na hata kupinga hatua ya wake zao kutaka kuwa na kazi
Lisa Njeru anasema ndoa yake ilivunjika na hana majuto baada ya mume wake Richard kukataa kabisa kwamba asifanye kazi . Pingamizi yake kubwa ilitokana na hali yake ya kuwa na wivu na kuhofia kwamba Lisa angekutana na mwanamme mwingine aliye ora huko kazini . Kila alipokuwa akitoka kazini ,Lisa anasema angempata mume wake amemngoja huku akiwa na maswali chungu nzima kuhusu watu aliokuwa amezungumza nao akiwa kazini
‘Angenichagulia nguo ambayo ningevaa nikienda kazini ….wakati mwingine nikijipodoa angesimama kando ya kioo akishangaa mbona najipodoa sana’ anasema Lisa
Anasema mwanzoni alifikiri labda hali ingeboreka na mume wake atulie kwa sababu hakuwa amewahi kufanya lolote la kumpa shauku au hofu kuhusu mapenzi yao . Lakini ilipofika wakati Lisa alipopandishwa cheo ili kuwa mkuu wa idara yake ,mume wake alimpa makataa ya kuacha kazi .
‘Aliniambia bila kusita kwamba amefika mwisho na nifanye uamuzi kati ya hiyo kazi na ndoa yangu’ Lisa anasema
Baada ya kujaribu kuzungumza na kakake za mume wake wajaribu kuongea na ndugu yao kuhusu mzozo huo Richard hakubadilisha msimamo na kwanza alikerwa Zaidi na hatua ya Lisa kuwahusisha jamaa zake katika suala hilo . Kwa takriban mwezi mmoja alikuwa amenuna na hakuna aliyekuwa akizungumz ana mwingine .
Baada ya kufirikia hatua atakayochukua ,Lisa alifanya uamuzi ,alifungisha virago vyake na kuondoka .Kilichomfanya kukwera Zaidi ni matamshi ya mume wake kwamba Lisa alikuwa na kiburi kwa sababu ya kazi na cheo chake . Alifahamu kwamba iwapo angeiacha kazi na tabia zile za Mume wake ,bado ndoa yao ingekuwa tu katika mizani na siku moja lingelipuka bomu ambalo lingemuacha bila ndoa au njia ya kujipa kipato . Je,Mbona kuna wanaume wasiotaka wake zao wafanye kazi?