(Picha) Dubai yaandaa Maonyesho ya Utalii jijini Nairobi

Washiriki watakuwa na nafasi ya kushiriki katika mchezo wa bahati nasibu wa Dubai.

Muhtasari

•Wadau kadhaa kutoka Dubai kwa sasa wanahudhuria hafla ya Idara ya Uchumi na Utalii ya Dubai katika hoteli ya MovenPick jijini Nairobi.

Mawakala wa usafiri kutoka Kenya wakiwa katika hafla ya Utalii ya Dubai mnamo Septemba 22.
Mawakala wa usafiri kutoka Kenya wakiwa katika hafla ya Utalii ya Dubai mnamo Septemba 22.
Image: WILFRED NYANGARESI

Wadau kadhaa kutoka Dubai kwa sasa wanahudhuria hafla ya Idara ya Uchumi na Utalii ya Dubai katika hoteli ya MovenPick jijini Nairobi.

Mawakala wa usafiri kutoka Kenya wakiwa katika hoteli ya MovenPick jijini Nairobi
Mawakala wa usafiri kutoka Kenya wakiwa katika hoteli ya MovenPick jijini Nairobi
Image: WILFRED NYANGARESI

Meneja wa Kanda Stela alisema kuwa wadau hao wapo nchini kwa ajili ya kuonyesha ofa walizonazo kwa wasafiri wa Afrika Mashariki.

wakati wa hafla ya utalii ya Dubai.
Mkurugenzi wa mauzo Chris Laghoutis Cluster wakati wa hafla ya utalii ya Dubai.
Image: WILFRED NYANGARESI

Hafla hiyo kawaida hufanyika kila mwaka kwa miaka mitano iliyopita.

"Kwa sababu ya janga la Covid-19, tulilazimika kuchukua mapumziko mwaka wa 2020 na kupanga upya," meneja wa konda alisema.

wakati wa hafla ya utalii ya Dubai jijini Nairobi.
Meneja Utalii wa Dubai wa Kanda Stella Obinwa wakati wa hafla ya utalii ya Dubai jijini Nairobi.
Image: WILFRED NYANGARESI

Siku ya leo, Alhamisi, washiriki watakuwa na nafasi ya kushiriki katika mchezo wa bahati nasibu wa Dubai.

wakati hotuba yake
Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Mawakala wa Usafiri wa Kenya Agnes Mucuha wakati hotuba yake
Image: WILFRED NYANGARESI

Zawadi hizo ni pamoja na safari iliyolipiwa kikamilifu ya kwenda Dubai.

wakati wa hotuba yake
Meneja Utalii wa Kanda wa Dubai Stella Obinwa wakati wa hotuba yake
Image: WILFRED NYANGARESI