LSK ndio inayoongoza maandamano hayo

LSK iko tayari kuingia majengo ya bunge baada ya kuwaarifu maspika

Maandamano hayo ya'Occupy Parliament' yanalenga kumshinikiza rais kulivunja bunge

Muhtasari
  •  Lsk inamtaka rais kuvunjilia bunge kama alivyoshauri jaji Mkuu 
  •   Havi anasema wabunge hawana tena maamlaka ya kuwaakilisha wakenya 

 

Wakili Nelson Havi
Nelson Havi Wakili Nelson Havi

 Rais wa  Chama cha mawakili nchini LSK Nelson Havi  ametibitisha kwamba  wamewaarifu maspika na makarani wa bunge la taifa na senate kuhusu nia yao ya kuingia majengo ya bunge hapo kesho.

 Kampeini hyo kwa jina  'Occupy Parliament'  ndio jitihada ya hivi punde ya LSK   kumshurutisha rais Uhuru Kenyatta  kulivunja bunge kama alivyoshauri jaji mkuu David Maraga .

  Mwingine aliyepewa taarifa  ya kwenda bungeni ni inspekta mkuu wa Polisi  ambaye LSK inamtaka atoe ulinzi wa maandamano hayo ya kuingia bungeni kuanzia saa nane unusu alasiri .

 

 Katika notisi yake LSK  inasema bunge limepoteza maamlaka ya kutunga sheria kwa nia ya wakenya .

 Kando  na LSK  makundi mengine yanayoshirikishwa katika mpango huo wa kuingia bungeni ni United Green Movement (UGM) na  Weare52pc.