- BBI yataka makamishna wapya wa IEBC
- Wasimamizi wa uchaguzi watasimamia tu uchaguzi mmoja mkuu
Ripoti ya BBI imependekeza kwamba maafisa wa tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC waondoke afisini kabla ya uchaguzi mkuu wa 2022
Ripoti hiyo ilikabidhiwa rais Uhuru Kenyatta na kiongozi wa ODM Raila Odinga siku ya jumatano huko Kisii .
Kamati ilyotayarisha ripoti hiyo imependekeza kuajiriwa kwa makamishna wapya wa IEBC kabla ya uchaguzi mkuu ujao ikisema hatua hiyo itaimarisha tume ya uchaguzi .
Kamati hiyo imesema panafaa kuwa na mwongozo wa wazi kuhusu majukumu ya makamishna hao na wajibu wa tume mpya kusimamia uchaguzi mkuu .
Kamati hiyo pia inapendekeza kwamba wafanyikazi wa IEBC waajiriwe kwa miakataba ya miaka mitatu ambayo inaweza kuongezwa kwa mujibu wa utendakazi wao .
Makamishna wa sasa wanaweza kusaidia katika utekelezaji wa mageuzi yaliyopendekezwa kwa kuweka mikakati ifaayo kwa matayarisho ya kuondoka afisini kwa hiari .
Kamati hiyo pia inataka maafisa wanaosimamia uchaguzi kuteuliwa kutumia mfumo unaotumiwa wakati wa kuwaajiri makamishna wa IEBC ikiwemo kuhusisha umma katika uteuzi wao
Pia maafisa wa kusimaia uchaguzi hawataajiriwa kwa muda na hawatasimamia zaidi ya uchaguzi mmoja
Pia kamati hiyo imependekeza kwamba maafisa wakuu wa IEBC wahojiwe upya na nyadhifa zao kubadilishwa ajina ili kuwa wakuu wa idara badala ya wakurugenzi .